Add parallel Print Page Options

Kuzaliwa kwa Yesu

(Mt 1:18-25)

Ulikuwa wakati ambapo amri ilitolewa na Kaisari Augusto kwamba watu wote wanaoishi katika utawala wote wa Rumi[a] wahesabiwe na kuorodheshwa[b] katika kumbukumbu za serikali. Orodha hii ilikuwa ya kwanza tangu Kirenio alipokuwa gavana wa Shamu. Kila mtu alikwenda katika mji aliozaliwa ili akahesabiwe na kuingizwa katika orodha hiyo.

Hivyo Yusufu alitoka Nazareti, mji uliokuwa katika jimbo la Galilaya na kwenda katika mji wa Bethlehemu uliokuwa katika jimbo la Uyahudi. Pia, mji huu ulijulikana kama mji wa Daudi. Yusufu alikwenda Bethlehemu kwa sababu alikuwa mzaliwa wa ukoo wa Daudi. Yusufu alijiandikisha akiwa pamoja na Mariamu kwani alikuwa tayari amemchumbia ili amwoe. Na Mariamu alikuwa mjamzito. Yusufu na Mariamu walipokuwa Bethlehemu, wakati wa Mariamu kujifungua ulifika. Akamzaa mwanawe wa kwanza. Akamvingirishia nguo vizuri, kisha akamlaza katika hori la kulishia mifugo.[c] Walimweka humo kwa sababu chumba cha wageni kilikuwa kimejaa.

Read full chapter

Footnotes

  1. 2:1 Rumi Au “dola ya ulimwengu ya Rumi”.
  2. 2:1 wahesabiwe na kuorodheshwa Yaani, “Sensa”, lengo hasa ilikuwa waorodheshwe katika kumbukumbu za serikali kwa ajili ya kulipa kodi.
  3. 2:7 hori la kulishia mifugo Sehemu au chombo cha kulishia mifugo. Pia katika mstari wa 12 na 16.